Manchester United inafanyakazi ya kuzikabili klabu nyengine za Ulaya kama vile Manchester City, Barcelona na Juventus, kumsaini mchezaji mwenye umri wa miaka 18 raia wa Brazil Gabriel Veron kutoka Palmeiras. (Sport via Star)
Mkufunzi wa Paris St-Germain Mauricio Pochettino anataraji kujiunga tena na kiungo wa kati Delle Alli. Maombi matatu ya Mabingwa hao wa Ufaransa kutaka kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 yamekataliwa , lakini Pochettino anaungwa mkono na klabu hiyo kuendelea kumnyatia. (The Athletic, subscription required)