INAWEZEKANA ikawa ni habari mbaya kwa mashabiki wa Simba baada ya kusikia winga wao machachari, Perfect Chikwende kutokuwa sehemu ya wachezaji watakaosafiri kwenda nchini DR Congo kucheza mechi ya hatua ya makundi katika Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AS Vita.
Simba inaondoka leo, huku mchezaji huyo akikosekana kutokana na awali tayari alishacheza Ligi hiyo akiwa na kikosi cha FC Platinums.