Edin Dzeko anatarajiwa kuondoka klabu ya Roma baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 raia wa Bosnia kutofautiana na mkufunzi Paulo Fonseca . (Goal)
Kurudi kwa Dzeko katika ligi ya Premia kunaweza kuwa suluhu kwa mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City huku akitarajiwa kuondoka katika mji huyo wa Itali, huku klabu za Everton na West ham zikimmezea mate. (Gazzetta Dello Sport via Mail)
Mkufunzi wa West Ham David Moyes anamtaka kiungo wa kati wa Manchester United Jesse Lingard baada ya mkufunzi wa Red Devil Ole Gunnar Solskjaer kukubali kumruhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kuondoka kwa mkopo. (Evening Standard)