Manchester City bado wanataka kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi, 33, msimu huu wa joto lakini wanajiandaa wakisubiri mpaka mwezi Machi au Aprili.(ESPN)
Mshambuliaji wa Inter Milan, Mbelgiji Romelu Lukaku, 27, na Muingereza anayekipiga Southampton Danny Ings,28, ni miongoni mwa wachezaji wanaotazamwa na Manchester City wakati huu ambapo klabu hiyo ikimtafuta mshambuliaji mpya. (Athletic - subscription required)
City itakabiliwa na ushindani wa Paris St-Germain katika kumnasa mshambuliaji Lukaku.(Calciomercato - in Italian)