Dar es Salaam. Nyota wapya waliosajiliwa na Simba, Perfect Chikwende na Taddeo Lwanga kwa mara ya kwanza wataonja ladha ya Ligi Kuu Tanzania Bara wakati timu hiyo itakapovaana na Dodoma Jiji FC katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, leo jioni.
Kusimama kwa Ligi Kuu Tanzania Bara ili kupisha maandalizi na ushiriki wa Taifa Stars kwenye mashindano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (Chan) kumesababisha nyota hao wachelewa kuichezea Simba kwenye ligi, lakini leo huenda wakaanza kuitumikia dhidi ya Dodoma Jiji.